Pata taarifa kuu

DRC yatiliana saini na MONUSCO kuhusu kuanza kuondoka kwa vikosi vya UN

Naiorbi – Waziri wa mambo ya nje wa DRC na kiongozi wa tume ya umoja wa Mataifa nchini humo, MONUSCO, wametiliana saini makubaliano ya kuanza kuondoka kwa walinda amani wa kimataifa waliokuwa kwenye taifa hilo kwa zaidi ya miongo miwili.

Kinshasa imekuwa ikiwatuhumu wanajeshi wa UN kwa kushindwa kurejesha usalama katika eneo la mashariki
Kinshasa imekuwa ikiwatuhumu wanajeshi wa UN kwa kushindwa kurejesha usalama katika eneo la mashariki REUTERS/Olivia Acland
Matangazo ya kibiashara

Waziri wa mambo ya nje, Christophe Lutundula, amesema makubaliano haya yanahitimisha rasmi ushirikiano wao na vikosi vya UN ambavyo tangu vimekuwa nchini humo vimeshindwa kurejesha usalama mashariki mwa nchi.

Katika hotuba aliyoitoa kwenye baraza la umoja wa mataifa mwezi Septemba mwaka huu, rais wa DRC, Felix Tshisekedi, alitoa wito wa kuharakishwa kwa mchakato wa kuondolewa kwa zaidi ya wanajeshi na polisi elfu 15 wa MONUSCO.

Walinda amani wa UN wamekuwa wakiwalinda raia kutokana na mashambulio yanayotekelezwa na makundi ya waasi mashariki mwa nchi hiyo
Walinda amani wa UN wamekuwa wakiwalinda raia kutokana na mashambulio yanayotekelezwa na makundi ya waasi mashariki mwa nchi hiyo REUTERS - STRINGER

Licha ya kuwa makubaliano hayo hayakuweka wazi tarahe ya mwisho ya kuondoka kwa vikosi hivyo, wadadisi wa mambo wanasema huenda ikawa ni baada ya uchaguzi wa mwezi ujao.

Mwezi uliopita, serikali ya Kinshasa, pia iliagiza kuondoka kwa wanajeshi wa kulinda amani kutoka kikosi cha jumuiya ya Afrika Mashariki, ifikapo mwisho wa mwaka huu.

Mwezi Julai mwaka wa 2022 baadhi ya waakazi wa DRC waliandamana wakitaka kuondoka kwa wanajeshi hao
Mwezi Julai mwaka wa 2022 baadhi ya waakazi wa DRC waliandamana wakitaka kuondoka kwa wanajeshi hao © AP Photo/Moses Sawasawa

Wakati huu kampeni za urais zikiwa zimeng’oa nanga, wagombea karibu wote wameonesha kuunga mkono kuondolewa kwa vikosi hivyo licha ya hali ya usalama kusalia kuwa tete katika maeneo mengi ya mashariki mwa nchi hiyo, suala hili likiwa miongoni mwa ajenga kuu za wagombea.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.