Tanzania na Indonesia kuimarisha uhushirkiano katika sekta mbalimbali
Nairobi – Tanzania na Indonesia, zimekubaliana kuimarisha uhusiano wa nchi hizo mbili katika sekta ya diplomasia, uchumu, afya na kilimo, na kutiliana saini mikataba kadhaa ya ushirikiano.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Rais Widodo amewasili Jumatatu jijini humu, leo akihitisha ziara ya siku mbili amekutana na Mwenyeji wake Ikulu kwa mazungumzo ya faragha.
Mara baada ya mazungumzo hayo, nchi hizo zilisaini hati saba za makubaliano ya ushirikiano katika kilimo, Indonesia kuiuzia Tanzania dawa, Miongoni mwa mengine.
Rais Samia anasema hatua hii inaimarisha uhusiano katika sekta mbalimbali.
“Tumekubaliana kwa pamoja kukuza biashara kwa kuzileta pamoja sekta za umma na binafsi na hapa tumelenga kushirikiana katika kilimo, viwanda, uwekezaji, Nishati Mafuta na gesi, Uvuni utalii na Sekta za Ukarimu, na kubadilishana maarifa na teknolojia. ” alieleza rais Samia.
Rais wa Tanzania Samia Hassan
Naye rais Widodo anasema uhusiano huu ulioasisiwa tangu mwaka 1955, una kila sababu ya kuimarika mara dufu hasa kwa kuongeza biashara baina ya nchi hizi
“Indonesia inafanya juhusi ili kuingia Makubaliano ya kibiashara ili kuimarisha biashara baina ya nchi zet ambazo kwa mwaka 2022 biashara iliongezeka kwa asilimia 2.7 pia kuchakata gesi asilia kuwa bidhaa kamili kama mbolea. ” Alisema rais Joko Widodo.
Rais Widodo kuhusu ushirikiano na Tanzania
Tanzania huuza mazao nchini Indonesia yakiwemo karafuu,tumbaku, karanga pamoja na madini mbalimbali huku Indonesia ikiiuzia Tanzania bidhaa za kemikali karatasi na nguo.
Steven Mumbi/Dar es salaam/Rfi Kiswahili