Pata taarifa kuu

Rais wa Hungary Katalin Novak anazuru Tanazania

Nairobi – Rais wa Hungary Katalin Novak amewasili nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi ya siku nne, ziara inayolenga kuimarisha uhusiano baina ya nchi hizo mbili. 

Rais wa Hungary Katalin Novak amewasili nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi ya siku nne
Rais wa Hungary Katalin Novak amewasili nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi ya siku nne © ikulu ya Tanzania
Matangazo ya kibiashara

Rais Novak, Rais wa kwanza mwanamke nchini humo anatembelea Tanzania kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia, kiuchumi na kibiashara Uhusiano uliodorora,  tangu kuasisiwa kwake miaka 1980. 

Tanzania na Hungary zimekuwa zikishirikiana katika sekta ya elimu,ambapo nchi ya Hungary imekuwa ikiwafadhili wanafunzi kwenda kusoma elimu ya juu katika ngazi ya shahada ya kwanza, Uzamili na Uzamivu. 

Wanafunzi hao kutoka Tanzania wamekua wakifadhiliwa katika Masomo ya Sayansi na Teknolojia,Uhandisi, Mawasiliano, Hisabati miongoni mwa mengine. 

Kwa Mujibu wa Shirika la Fedha Duniani IMF, nchi ya Hungary ni ya  57 Duniani kwa ukuaji kiuchumi kati ya nchi 188 na kuwa miongoni mwa nchi zenye uchumi uliomarika Zaidi barani Ulaya. 

Ziara hiyo inatarajiwa kutamatika Julai 20 mwaka huu mara baada ya kuzungumza na mwenyeji wake Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.