Pata taarifa kuu

Uganda: Kupitishwa kwa sheria kandamizi kunawaingiza mashoga katika hofu

Bunge la Uganda hivi majuzi lilipitisha sheria ya kupinga ushoga inayoelezwa kuwa moja ya sheria kandamizi zaidi duniani, inayowatia wasiwasi watetezi wa haki za watu wa jamii ya LGBT+.

Kutoka mpaka wa Kenya hadi Afrika Kusini kupitia Ulaya na Amerika Kaskazini, Waganda wengi tayari wamechukua njia ya uhamishoni muda mrefu kabla ya sheria hiyo kupitishwa.
Kutoka mpaka wa Kenya hadi Afrika Kusini kupitia Ulaya na Amerika Kaskazini, Waganda wengi tayari wamechukua njia ya uhamishoni muda mrefu kabla ya sheria hiyo kupitishwa. AFP PHOTO/ ISAAC KASAMANI
Matangazo ya kibiashara

"Watatukamata kwa sababu siwezi kujifanya nisivyo," amesema Alex, 19, mpenzi wa jinsia moja nchini Uganda, ambapo hivi majuzi bunge lilipitisha muswada wa kupinga ushoga unaoelezwa kuwa mojawapo ya kandamizi zaidi duniani.

Sheria hii inayojulikana rasmi kama "Sheria ya Kupambana na Ushoga 2023", bado haijatiwa saini na Rais Yoweri Museveni, ambaye ameongoza nchi kwa mkono wa chuma tangu mwaka 1986. Umoja wa Mataifa na Marekani zimetaka rais Museveni kufutilia mbali sheria hityo.

Sheria hiyo ilipitishwa na bunge mnamo Machi 21 katika kikao kizito cha Baraza la Bunge. Lakini kulingana na wanaharakati wa haki za LGBT+, ikiwa Yoweri Museveni ataidhinisha sheria hii, mtu yeyote anayejihusisha na vitendo vya mapenzi ya jinsi moja anaweza kuhukumiwa kifungo cha maisha jela. Na adhabu ya kifo hutolewa katika kosa hili litarudiwa.

Ikijumuishwa katika sheria za Uganda, hukumu ya kifo haijatumika kwa miaka mingi. Faraja kidogo kwa wanachama wa jamii ya LGBT+ nchini Uganda, kama vile Alex ambaye jina lake, kama wengine, limebadilishwa kwa sababu za usalama.

Kutoka mpaka wa Kenya hadi Afrika Kusini kupitia Ulaya na Amerika Kaskazini, Waganda wengi tayari wamechukua njia ya uhamishoni muda mrefu kabla ya sheria hiyo kupitishwa.

Sheria ya awali ya kupinga ushoga iliyotangazwa mwaka wa 2014 na Bw. Museveni ilizisukuma nchi za Magharibi kupunguza misaada yao ya kimataifa. Mahakama ya Katiba ya Uganda hatimaye ilibatilisha sheria hii kwa kasoro ya kiufundi wakati wa upigaji kura. Yoweri Museveni sasa lazima asuluhishe kati ya kuungwa mkono na wakazi wake kwa sheria hii, na hatari za kutengwa kimataifa.

Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu Volker Türk alishutumu sheria "pengine miongoni mwa sheria mbaya zaidi za aina yake duniani". Marekani, kwa upande wake, ilitishia mamlaka mjini Kampala kwa "athari", hasa za kiuchumi. Katika miezi ya hivi karibuni, viongozi wa kidini na kisiasa wameshiriki nadharia za njama zisizo na msingi kuhusu wapenzi wa jinsi moja, ikiwa ni pamoja na shutuma za kushambulia watoto kwa amri ya nguvu za giza za kimataifa.

"Waganda wamekuwa na msimamo mkali, hali ni mbaya zaidi" kuliko mwaka 2014, Franck Mugisha, mkurugenzi mtendaji wa Sexual Minorities Uganda, shirika la kutetea haki za wapenzi wa jinsi moja ambalo shughuli zake zimesitishwa na mamlaka, aliliambia shiria la habari la AFP.'mwaka jana.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.