Pata taarifa kuu
SUDANI KUSINI-USALAMA

Rais wa Sudan Kusini aanza kutia katika vitendo mkataba wa aman iwa 2018

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir, ameunda komandi mpya  ya jeshi la pamoja, inayojumuisha vikosi vya upinzani, ikiwa ni utekelezaji wa kipengele muhimu katika mkataba wa amani wa mwaka 2018.

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir (kushoto) na makamu wake, kiongozi wa zamani wa waasi Riek Machar (kulia) mjini Juba Februari 20, 2020 wakati wa mkutano wa pamoja na waandishi wa habari.
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir (kushoto) na makamu wake, kiongozi wa zamani wa waasi Riek Machar (kulia) mjini Juba Februari 20, 2020 wakati wa mkutano wa pamoja na waandishi wa habari. REUTERS/Jok Solomun
Matangazo ya kibiashara

Hatua hii inakuja baada ya mapigano ya hivi karibuni kati ya vikosi vya Kiir na Machar, kusababisha zaidi ya watu Elfu 14 kuyakimbia makwao.

Baada ya hatua hii, wanajeshi na polisi watapata mafunzo ya pamoja ndani ya miezi miwili, kwa mujibu wa makubaliano hayo.

Kulikuwa na wasiwasi kuhusu kutokea mapigano mapya nchini Sudan Kusini, kati ya vikosi tiifu kwa Salva Kiir na Riek Machar, kila mmoja akimtuhumu mwingine kwa kukiuka mkataba wa amani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.