Mchakato wa uteuzi wa Katibu mkuu wa Jumuiya ya Afrika mashariki mashakani
Mchakato wa mataifa wanachama kwenye jumuiya ya Afrika Mashariki kujaza nafasi ya katibu mkuu wa jumuiya ya Afika mashariki, Liberat Mfumukeko anayemaliza muhula wake mwezi Aprili unazidi kuibua hisia kali ambapo mataifa wanachama yanaendelea kuvutana kuelekea kukamilika mchakato huo.
Imechapishwa:
Hali hii imejitokeza baada ya Kenya na Sudan Kusini, kutangaza azma ya kuteua mwaniaji kwenye nafasi hiyo.
Kwa kawaida nafasi hiyo huwa ni ya kupokezana kati ya mataifa wanachama na japo zamu ya Kenya kujaza nafasi hiyo ,Sudan Kusini ,taifa la hivi majuzi kujiunga na jumuiya limetangaza lipo kwenye kinyanganyiro hicho.
Hii ni licha ya Sudan Kusini kutuhumiwa kuwa na deni kubwa la ada ya uanachama na bado haijapitisha sheria hitajika za kuwezesha biashara huru na umoja wa forodha.
Wanaotazamiwa kuwania kiti hicho kutoka Kenya ni katibu mtendaji katika wizara ya mambo ya nje Ababu Namwamba, Waziri wa ustawi wa jumuiya ya Afrika Mashariki Aden Mohammed na waziri wa michezo Amina Mohammed.
Sudan Kusini kwa upande wake ,imempendekeza aliyekuwa waziri wa fedha Aggrey Tisa Sabuni