Pata taarifa kuu

UN: Afrika itabidi ibadilishe mfumo wake wa vyoo na mafuŕiko ya mara kwa mara

Ubinadamu 'umevunja mzunguko wa maji', 'dutu yake muhimu'. Maneno yaliyosemwa mjini New York na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, katika siku ya pili ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Maji, bara la Afrika likitazamwa kwa umakini. Afrika inakabiliwa zaidina matatizo ya upatikanaji wa maji.

Mtoto akijaza kwenye dumu maji katika kitongoji duni cha Kisenyi, Kampala, Uganda mwaka wa 2019. Kulingana na Umoja wa Mataifa, ni asilimia 30 tu ya wakazi wa Kusini mwa Jangwa la Sahara wanapata chanzo salama cha maji ya kunywa.
Mtoto akijaza kwenye dumu maji katika kitongoji duni cha Kisenyi, Kampala, Uganda mwaka wa 2019. Kulingana na Umoja wa Mataifa, ni asilimia 30 tu ya wakazi wa Kusini mwa Jangwa la Sahara wanapata chanzo salama cha maji ya kunywa. Photothek via Getty Images - Ute Grabowsky
Matangazo ya kibiashara

Tangu mwaka 2010, kumekuwa na ghasia za kiu mara arobaini zaidi barani Afrika. Hali ni nzuri zaidi nchini Côte d'Ivoire na Mali kuliko Cameroon au Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Lakini kwa wastani, asilimia 40 ya wakazi wa Afrika hawana uhakika wa kupata maji safi.

Kadiri idadi ya watu inavyoongezeka, mabadiliko ya Tabia nchi yanaongezeka na kuzidisha ukame, kama ilivyo katika Afrika Mashariki hivi sasa. Katika baadhi ya maeneo ya Kenya, bei ya maji imeongezeka mara tano.

Kwingineko, katika Afrika ya Kati na Sahel, mafuriko katika miezi ya hivi karibuni yamechafua vyanzo vya maji safi. Katika hali moja kama ilivyo kwa nyingine, ukosefu wa maji safi, husababisha 80% ya magonjwa, husababisha kuibuka tena kwa kipindupindu katika nchi kumi na tano za Afrika. Takriban 70% ya Waafrika wamenyimwa mfumo wa usafi wa mazingira, yaani vyoo na kushughulikia maji taka.

Haja ya marekebisho na uwekezaji

Sekta ya maji na usafi wa mazingira kwa hivyo italazimika kubadilika kwa ujumla, anaelezea, kutoka New York, mkurugenzi mkuu wa Mpango wa Mshikamano wa Maji, Christophe Le Jalle.

Miaka michache iliyopita, zaidi ya saa thelathini, kulikuwa na milimita mia kadhaa [ya mvua] huko Ouagadougou. Ni mfumo gani unaweza kushughulikia hilo? Ni vigumu sana. Ikiwa kunazungumziwa kuhusu usafi wa mazingira, hizi mara nyingi ni aina za usafi zisizo za pamoja, ni mashimo. Kunapokuwa na mafuriko, mashimo haya hufurika kwa matatizo ya usafi ambayo husababishwa na hili [...] Suluhisho ni kwamba angalau ngazi za kwanza za kuta za choo ziwe ngumu, kwa hiyo simenti [. ..]
Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.