Pata taarifa kuu
AFGHANISTAN

Ni kosa kwa wanawake kutembea bila kufunika nyuso zao- Taliban

Uongozi wa kundi la Taliban nchini Afghanistan, umewaagiza wanawake kwenye taifa hilo kufunika nyoso zao kwa burqa wakati wakiwa katika maeneo ya umaa.

Mpiganaji wa Taliban akiaandamana na wanawake katika mji wa Kaboul
Mpiganaji wa Taliban akiaandamana na wanawake katika mji wa Kaboul © AP - Ebrahim Noroozi
Matangazo ya kibiashara

Agizo hili limetajwa  kuwa moja wapo ya marshati makali zaidi kutangazwa na kundi hilo dhidi ya wanawake nchini Afghanistan  tangu kuchukua uongozi wa taifa hilo mwaka jana, Baadhi ya sheria zinazotekelezwa na wapiganaji hao zimekuwa zikikashifiwa vikali na  jamii ya kimataifa pamoja na  raia kwenye taifa hilo.

Haibatullah Akhunzada, Mkuu wa kundi la Taliban katika taarifa yake iliyosomwa wakati wa halfa iliyofanyika jijini Kabul siku ya jumamosi, ametaja kitendo cha wanawake kujifunika kutoka kichwani hadi kwenye miguu kuwa kitendo kinachoaashiria heshima katika jamii  na kinalinagana na tamaduni.

Agizo hilo aidha linaeleza kuwa iwapo baba au mtu mwenye jinsia ya kiume na ambaye ni wa karibu  na mwanamke atakayepatikana katika maeneo ya umma bila ya kujifunika uso wake, “atatembelewa” na kufungwa jela au hata kuaachishwa kazi kwa wale walioaajiriwa na serikali.

Tangu kuchukua madaraka, Taliban wamerejesha baadhi ya sheria zikiwemo kudhibiti uhuru wa watu kutembea sheria zinazowalenga wanawake pakubwa hali inayorejesha picha ya utawala wao katika  miaka ya 1990.

Kwa kipindi cha miezi michache iliyopita, viongozi wa Taliban wametangaza marsharti na vikwazo vingi kwa raia wa Afghanistan licha ya kukashifiwa na jamii ya kimataifa.

Mwezi disemba mwaka jana, Taliban ilitangaza sheria inayowazuia wanawake kwenda umbali wa kilomita 72 bila ya kuaandamana na mtu wa jinsia ya kiume.

Marekani na mataifa mengine yamesitisha msaada kwa Afghanistan tangu wapiganaji wa Taliban walipochukua uongozi mwezi agosti na hata kuwaondoa wanajeshi wake nchini humo. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.