Hong Kong: Majadiliano yaanza juu ya mswada tata kuhusu usalama wa raia
Bunge la Hong Kong, ambalo halina vyama vya upinzani, linaanza majadiliano leo Jumatano juu ya sheria tata kuhusu usalama wa raia inayolenga kukabiliana na mambo mbalimbali, ambayo makampuni makubwa ya teknolojia yana hofu kwa inaweza kuzorotesha shughuli mbalimbali katika eneo hilo.
Imechapishwa:
Mashirika yanayotetea haki za binadamu na makampuni ya teknolojia yanayokosoa mradi huo, yakisema kuwa hatua hizo zinaweza kutumiwa kuwalinda walio madarakani na kulenga mashirika ya kiraia.
Watetezi wa sheria hiyo wanasema ilikuwa imechelewa kushughulikia shida ambayo imeongezeka tangu maandamano makubwa ya wanademokrasia ya 2019.
Serikali ya Hong Kong haina upinzani wowote rasmi baada ya wabunge wanaotetea demokrasia kujiuzulu kwa wingi mwaka jana kupinga hatua ya kuwatimuwa wenzao kwenye nafasi zao. Hii inamaanisha kuwa mswada huo sheria unaweza kupitishwa haraka.