Pata taarifa kuu
MAREKANI-KOREA KASKAZINI-USALAMA

Marekani yaionya Korea Kaskazini

Katika mahojiano na shirika la habari la ABC, Mshauri wa Rais Donald Trump wa masuala ya usalama, Herbert Raymond McMaster Jeneral Mc Master amesema kuwa Marekani na China zinaelekea kupoteza uvumilivu na Korea Kaskazini.

Kora Kaskazini yaendelea kufanya majaribio ya makombora yake ya masafa marefu licha ya vitisho vya Umoja wa Mataifa.
Kora Kaskazini yaendelea kufanya majaribio ya makombora yake ya masafa marefu licha ya vitisho vya Umoja wa Mataifa. U.S. Department of Defense, Missile Defense Agency/Handout via R
Matangazo ya kibiashara

Herbert Raymond McMaster amesisitiza kuwa majaribio ya makombora ya hivi karibuni, yanaonyesha tabia ya vitisho ya Korea Kaskazini, huku akibaini kuwa kuna makubaliano ya kimataifa, ikiwemo China, kuhakikisha tabia hii haiendelei.

Herbert Raymond McMaster amesema makubaliano yanayojitokeza dhidi ya tabia ya vitisho ya Korea Kaskazini kwa sasa yanaijumuisha China.

Wakati huo huo Rais Trump ameweka wazi kuwa Marekani na washirika wake hawatokubali kuona utawala wa vitisho dhidi ya silaha za nyuklia.

Makamu wa Rais wa Marekani Mike Pence, ambaye anazuru Korea Kusini amesema uhuru utashinda.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.