Pata taarifa kuu

Rais mpya wa Peru awataka wananchi kumpa muda wa kurosha kutokomeza rushwa

Nchini Peru, rais mpya Dina Boluarte ameanza kupata shinikizo za kuunda serikali, siku moja baada ya kuapishwa katika nafasi hiyo, kufuatia kuondolewa madarakani na kukamatwa kwa mtangulizi wake Pedro Castillo, baada ya jaribio la kulivunja bunge na kutaka kutawala kwa mkono wa chuma.

Rais wa mpito wa Peru Dina Boluarte, ambaye alitakiwa na Bunge la Congress kuchukua wadhifa huo baada ya bunge kuidhinisha kuondolewa kwa Rais Pedro Castillo katika kesi ya kumuondoa madarakani, huko Lima, Peru Desemba 7, 2022.
Rais wa mpito wa Peru Dina Boluarte, ambaye alitakiwa na Bunge la Congress kuchukua wadhifa huo baada ya bunge kuidhinisha kuondolewa kwa Rais Pedro Castillo katika kesi ya kumuondoa madarakani, huko Lima, Peru Desemba 7, 2022. REUTERS - SEBASTIAN CASTANEDA
Matangazo ya kibiashara

Baada ya kuapishwa kuongoza taifa hilo la America Kusini, katika kipindi hiki cha mvutano mzito wa kisiasa, ameomba, muda ili kupambana na ufisadi na kuimarisha uongozi wa nchi hiyo. 

Ninachokiomba ni kupewa muda ili nipambane na rushwa na kuliokoa taifa letu kutokana  na uongozi mbaya.

Rais huyo mpya, anatarajiwa kukaa madarakani, hadi mwezi wa Julai 2026 wakati muhula wa mtangulizi wake, Pedro Castillo, utakapomalizika. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.