Pata taarifa kuu
MEXICO-USALAMA

Mexico: Mwandishi wa habari Alfredo Cardoso Echeverria auawa kwa risasi

Mkurugenzi wa tovuti ya habari huko Acapulco, katika jimbo la Guerrero, kusini mwa Mexico, alifariki Oktoba 31 hospitalini, siku mbili baada ya kupatikana akiwa amejeruhiwa vibaya kwa risasi, mamlaka imetangaza.

Mkurugenzi wa tovuti ya habari huko Acapulco, kusini mwa Mexico, alifariki Oktoba 31 hospitalini, siku mbili baada ya kupatikana akiwa amejeruhiwa vibaya na risasi.
Mkurugenzi wa tovuti ya habari huko Acapulco, kusini mwa Mexico, alifariki Oktoba 31 hospitalini, siku mbili baada ya kupatikana akiwa amejeruhiwa vibaya na risasi. AFP/File
Matangazo ya kibiashara

"Ninapaswa nitoe rambirambi zangu kwa familia ya mwanahabari Alfredo Cardoso Echeverria, mwanzilishi wa tovuti ya habari ya Las Dos Costas, kwa mauaji haya ya kusikitisha," Evelyn Salgado, gavana wa jimbo la Guerrero, alisema kwenye mtandao wa kijamii.

Kulingana na shirika la Wanahabari Wasio na Mipaka (RSF), Bw. Cardoso, ambaye familia yake ilipokea vitisho, alitekwa nyara Alhamisi (Oktoba 28) na watu waliokuwa wamejifunika nyuso zao ambao walivamia nyumba yake.

Alipatikana siku iliyofuata akiwa amejeruhiwa kwa risasi tano kwenye gari lake, vyombo vya habari vya nchini Mexico vimeripoti. Alikimbizwa hospitalini haraka, mwanahabari huyo alifariki dunia siku ya Jumapili.

Takriban wanahabari saba wameuawa mwaka huu wa 2021 nchini Mexico. Lakini, haijbainishwa kuwa vifo vyao vilihusiana na kazi yao.

Mexico, ikiwa na zaidi ya waandishi wa habari mia moja waliouawa tangu mwaka 2000 kulingana na takwimu kutoka Tume ya Haki za Kibinadamu, inachukuliwa kuwa moja ya nchi hatari zaidi kwa wale wanaofanya kazi ya kuelimisha umma.

Waandishi wanane waliuawa mnamo 2020, RSF imekumbusha. Zaidi ya 90% ya mauaji ya waandishi wa habari hayaadhibiwi, mashirika yanayotetea uhuru wa kujieleza yanabaini.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.