Venezuela yalaani "utekaji nyara" wa wanajeshi wake 8
Waziri wa Ulinzi wa Venezuela ameshutumu "utekaji nyara" wa wanajeshi wanane na kundi la uhalifu lenye silaha cha makosa ya Colombia, kusini magharibi mwa Venezuela, karibu na Colombia, eneo ambalo mapigano na jeshi yanafanyika tangu Machi 21.
Imechapishwa:
"Wakati wa mapigano, askari wanane wa kitaalam walikamatwa. Tulipokea uthibitisho wa maisha mnamo Mei 9. Tunalaani kwa jamii ya kimataifa [...] utekaji nyara wa wanajeshi hawa," Waziri Vladimir Padrino Lopez akibaini kwamba uamizi huo iliyosomwa kwenye runinga ikithibitisha tangazo lililotolewa Jumatatu na NGO ya haki za binadamu.
Lakini kundi la waasi la mrengo wa kushoto katika eneo hilo linashukiwa kutekeleza utekaji nyara huo.
Maelfu ya wanajeshi na maafisa wa polisi wanahusika katika juhudi za kuwaokoa wanajesi hao.