Coronavirus: Idadi ya vifo kutokana na COVID -19 yakaribia 400,000 Brazil
Brazil inatarajia kurekodi vifo vya 400,000 wiki hii kutokana na COVID-19, baada ya wizara ya afya siku ya Jumatano kuripoti vifo vipya 3,163 kutokana na COVID-19 kati ya kipindi cha saa 24, na kusababisha idadi rasmi ya vifo kfikia 398,185.
Imechapishwa:
Brazil inatarajia kufikisha idadi kubwa ya vifo duniani, sawa na ile ya Marekani, ambayo imerekodi zaidi ya vifo 570,000 kwa jumla.
Mgogoro wa COVID-19 nchini Brazil ulishindwa kudhibitiwa katika miezi ya hivi karibuni, pamoja na vizuizi visivyo halali kuhusu watu kutembea na aina mpya ya kirusi cha Corona kinachoambukia haraka.
Rais wa Brazil Jair Bolsonaro amekosolewa vikali kwa kudharau hatari za virusi, kwa kupuuzia uvaaji wa barakoa na kupendekeza tiba ambazo hazijathibitishwa.
Wizara ya afya ya Brazil pia imeripoti visa vipya 79,726 vya maambukizi vilivyothibitishwa siku ya Jumatano, na kufanya jumla visa vya maambukizi kufikia 14,521,289.