Bunge lapitisha azimio la kuzuia hatua ya kijeshi ya Trump dhidi ya Iran
Baraza la Wawakilishi linalodhibitiwa na chama cha Democratic limepitisha azimio siku ya Alhamisi ya kuzuia mamlaka ya Donald Trump kuzindua oparesheni za kijeshi dhidi ya Iran, nakala ambayo ni ishara lakini ni maudhi kwa rais Trump.
Imechapishwa:
Kumhimiza Donald Trump "kusitisha" hatua zote za kijeshi dhidi ya Iran kwa kutoungwa mkono na Baraza la Congress, azimio hilo limepitishwa kwa kura 224 dhid ya 194.
Inaonekana kuwa azimio hilo litapelekwa mbele ya Bunge la Seneti, linalodhibitiwa na chama cha Republican ambalo linamuunga mkono kwa idadi kubwa ya wajumbe Donald Trump.
Azimio hilo linalenga kulipa Baraza la Congress nguvu ya kutoa kibali cha shambulio lolote dhidi ya Iran, isipokuwa pale tu patakapokuwa na shambulio la ghafla dhidi ya Marekani.
Kwa sasa hakuna upande kati ya Iran na Marekani ambao umetamka kuwa utaendelea na mashambulizi.