Pata taarifa kuu
VENEZUELA-MAANDAMANO-USALAMA

Rais Maduro ataka katiba mpya, upinzani wakataa

Siku ya Jumatatu rais wa Venezuela Nicolas Maduro alitoa wito wa kuundwa kwa Bunge la Katiba, ambalo litakua na mamlaka ya kuandika katiba mpya. Licha ya tangazo hilo, maandamano yaliendelea kushuhudiwa katika mitaa mbalimbali nchini Venezuela.

Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro, amesema Bunge la katiba litaundwa na raia wa kawaida.
Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro, amesema Bunge la katiba litaundwa na raia wa kawaida. Fuente: Reuters.
Matangazo ya kibiashara

Rais Maduro amesema taasisi hiyo mpya itaundwa na raia wa kawaida na kuachana na bunge la kitaifa lenye wabunge wengi kutoka upinzani.

Wakati huo huo kiongozi wa upinzani Henrique Capriles amesema taasisi hiyo itakua na malengo ya kufuta katiba ya nchi.

Hayo yakijiri maelfu ya wafuasi wa upinzani walimiminika siku ya Jumatatu mitaani wakidai kufanyike uchaguzi wa mapema, hata hivyo makabiliano makali yalishuhudiwa kati ya waandamanaji na vikosi vya usalama.

maelfu ya wafuasi wa upinzani waandamana siku ya wafanyakazi duniani, Mei 1, 2017, Caracas.
maelfu ya wafuasi wa upinzani waandamana siku ya wafanyakazi duniani, Mei 1, 2017, Caracas. REUTERS/Christian Veron

Venezuela imeendelea kukumbwa na maandamano ya upinzani wakitaka rais Nicolas maduro ajiuzulu mara moja.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.