VENEZUELA-MAANDAMANO-USALAMA
Rais Venezuela anyooshewa kidole cha lawama
Marekani na Umoja wa Ulaya zimeshtumu rais wa Venezuela Nicolas Maduro kwa kuwaminya wapinzani.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Rais Donald Trump amesema Venezuela imepoteza mwelekeo kutokana na maandamano yanayoendela kushinikiza kujiuzulu kwa rais Maduro.
Maandamano nchini Venezuela yamesababisha vifo vya watu 28, huku serikali ikiyashtumu Mataifa ya Magharibi kwa kuchochea maandamano hayo.
Hata hivyo upinzani umeapa kuendelea na maandamano hadi rais wa Venezuela, Nicolas Maduro atapojiuzulu.
Hivi karibuni, Rais Maduro aliomba mazungumzo na upinzani ili kukomesha maandamano hayo.