MAREKANI-UJERUMANI
Trump na Merkel wakutana kuzungumzia Usalama
Raisi wa Marekani Donald Trump amemkaribisha Kansela wa Ujerumani Angela Merkel katika ikulu ya white house kwa mara ya kwanza tangu aingie madarakani.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Viongozi hao wenye misimamo tofauti wanakutana na kufanya mazungumzo kwa mara ya kwanza tangu Trump kuingia madarakani.
Miongoni mwa agenda zinazotajwa kupewa kipaumbele katika mazungumzo ya viongozi hao ni pamoja na mapambano dhidi ya kundi la kijihadi la islamic state,kuimarisha jeshi la NATO na utatuzi wa mzozo wa Ukraine na Urusi.
Katika mkutano na waandishi wa habari Merkel amesema imekuwa jambo zuri kukutana na kuzungumza ana kwa ana na sio kuzungumziana.