Maambukizi ya virusi vya Corona yaanza kupungua Afrika
Idadi ya maambukizi ya virusi vya Corona barani Afrika imeanza kushuka kuanzia wiki iliyopita,hii ikitafsiriwa kuwa ishara nzuri ya bara hili kufanikiwa katika mapambano dhidi ya janga hili.
Imechapishwa:
Mkurugenzi wa kituo cha kudhibiti magonjwa barani Dkt John Nkengasong amesema ingawaje ugonjwa huo ulikuwa hatari ,kuna matumaini ya kuushinda.
Afrika kufikia sasa ina zaidi ya maambukizi milioni moja ,Afrika Kusini ikichangia kiasi kikubwa.
Kwa upande mwingine shirika la Afya Duniani WHO limesema bara ulaya linaweza kupambana na maambukzi mapya ya Corona pasipo kurejesha amri ya kusalia manyumbani.
Kuanzia Alhamisi, Italia, Ufaransa na Uhispania ,zimeshuhudia ongezeko la kasi ya maambukizi ya virusi hivyo.