Pata taarifa kuu

Togo: Ecowas kujaribu kupata suluhu ya kisiasa baada ya mabadiliko ya katiba

Ujumbe wa Jumuiya ya Kiuchumi kutoka nchi za Afrika Magharibi ECOWAS umekwenda nchini Togo, kujaribu kupata suluhu ya kisiasa kufuatia mabadiliko ya katiba yaliyozua hali ya sintofahamu kati ya wanasiasa.

[Picha] Bendera ya Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) mjini Accra, Ghana, Machi 25, 2022.
[Picha] Bendera ya Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) mjini Accra, Ghana, Machi 25, 2022. REUTERS - FRANCIS KOKOROKO
Matangazo ya kibiashara

ECOWAS imesema imetuma ujumbe wake, kufanya mashauriano na wadau wote, wakati huu nchi hiyo ikijiandaa kushiriki kwenye uchaguzi wa wabunge tarehe 29 mwezi huu.

Ujumbe huo unaongozwa na aliyekuwa mjumbe wa Umoja wa Afrika (AU) nchini Mali na ukanda wa Sahel Maman Sambo Sidikou, ambaye anatarajiwa kutamatisha ziara yake siku ya Jumamosi.

Bango linaloonyesha picha ya Rais wa Togo Faure Gnassingbé, aliyekuwa mgombea urais wa chama cha UNIR, mjini Lomé mnamo Februari 19, 2020.
Bango linaloonyesha picha ya Rais wa Togo Faure Gnassingbé, aliyekuwa mgombea urais wa chama cha UNIR, mjini Lomé mnamo Februari 19, 2020. © Reuters / Luc Gnago

Hali ya sintofahamu ya kisiasa inaendelea baada ya mwezi uliopita, wabunge kupitisha mabadiliko ya katiba kubadilisha mfumo wa uongozni nchini humo ambapo rais atachaguliwa na wabunge na sio wananchi, kwa muhula wa miaka sita.

Soma piaTogo yahirisha uchaguzi wa wabunge hadi Aprili 29

Wanasiasa wa upinzani, viongozi wa dini na mashirika ya kiraia, wanasema huu ni mpango wa rais Faure Gnassingbe, ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 2005 kuendelea kusalia madarakani.

Hillary Ingati- RFI-Kiswahili.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.