Senegal: Wafuasi wa Diomaye Faye wadai ushindi, kambi tawala haikubaliani
Wafuasi wa Bassirou Diomaye wanasherehekea na kudai ushindi wa mgombea wao huku matokeo rasmi ya uchaguzi wa urais wa Jumapili bado hayajatangazwa. Wengi wa wagombea pia wamempongeza mpinzani huyo lakini bado mgombea wa kambi tawala anasema anasema bado hajakubali kushindwa na ameahidi kuzungumza leo Jumatatu.
Imechapishwa:
Vyombo vya habari nchini Senegal vinasema mwanasiasa wa upinzani Bassirou Diomaye Faye anaonekana kuongoza katika uchaguzi wa urais nchini Senegal, lakini kambi ya tawala imehakikisha kuwa kutakuwa na duru ya pili.
Baada ya miaka mitatu ya fadhaa na mgogoro, Wasenegal bado wanasubiri Jumatatu kujua matokeo ya uchaguzi ambayo yataamua kati ya mwendelezo na labda mabadiliko makubwa. Wanasalia kutokuwa na uhakika juu ya hitaji la duru ya pili, ambayo hakuna tarehe iliyotangazwa.
Matokeo rasmi ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili yatatangazwa baadaye wiki hii. Tume ya kitaifa ya uchaguzi ina hadi Ijumaa kutangaza matokeo ya muda, kabla ya kuthibitishwa na Mahakama ya Katiba.
Idadi kamili ya kura zilizopigwa inahitajika ili kushinda katika duru ya kwanza. Vinginevyo, washindi wawili wa kwanza watashindana katika duru ya pili.
Matokeo yaliyochapishwa kwenye vyombo vya habari na kwenye mitandao ya kijamii yanamweka mgombea Bassirou Diomaye Faye mbele ya yule wa kambi tawala, Amadou Ba, na kwa mbali sana kuliko wengine.
Angalau wagombea saba kati ya 17 walimpongeza Bw Faye kwa kuzingatia matokeo ya muda yaliyochapishwa na vyombo vya habari.