Pata taarifa kuu

Senegal: Matokeo ya uchaguzi wa urais yaendelea kusubirwa

Nairobi – Nchini Senegal, matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika jana yanaendelea kusuburiwa  wakati huu ripoti zikisema Bassirou Diomaye Faye mgombea mkuu wa upinzani anaongoza.

Wafuasi wa Faye wameanza kusherehekea mapema, wakati huu kura zikiendelea kuhesabiwa na kujumuishwa.
Wafuasi wa Faye wameanza kusherehekea mapema, wakati huu kura zikiendelea kuhesabiwa na kujumuishwa. AFP - MUHAMADOU BITTAYE
Matangazo ya kibiashara

Faye anaongoza kwa mujibu wa matokeo ya awali  yaliyotangazwa kutoka kwenye vituo mbalimbali vya kupigia kura, dhidi ya aliyekuwa Waziri Mkuu Amadou Ba, ambaye anaungwa mkono na serikali.

Washirika wa karibu wa Ba, wanasema kwa namna matokeo yalivyo wana uhakika kuwa uchaguzi huo utakwenda kwenye mzunguko wa pili.

Bassirou Diomaye Faye mgombea mkuu wa upinzani anaongoza kwa mujibu wa matokeo ya awali
Bassirou Diomaye Faye mgombea mkuu wa upinzani anaongoza kwa mujibu wa matokeo ya awali AFP - SEYLLOU

Wafuasi wa Faye wameanza kusherehekea mapema, wakati huu kura zikiendelea kuhesabiwa na kujumuishwa, huku wagombea saba wakiongozwa na Anta Babacar Ngom, wakimpongeza kwa kuibuka mshindi .

Iwapo Faye anayeungwa mkono na Ousame Sonko, mwanasiasa wa upinzani mwenye ushawishi, aliyezuiwa kuwania urais, atathibtishwa mshindi, atakuwa na kazi kubwa ya kufanya mageuzi makubwa nchini Senegal na kuongoza vita dhidi ya rushwa na kuhakikisha kuwa anatenegeza mazingira ya kuundwa kwa ajira hasa kwa vijana.

Mshindi anatarajiwa kumrithi rais Sall anayeondoka madarakani
Mshindi anatarajiwa kumrithi rais Sall anayeondoka madarakani AP - Mosa'ab Elshamy

Ba naye amekuwa akiahidi kuendeleza uongozi wa rais Macky Sall ambaye anaondoka madarakani.

Tume ya Uchaguzi inatarajiwa kumtangaza mshindi kabla siku ya Ijumaa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.