Pata taarifa kuu

Sudan: Shule zafungwa kutokana na joto kali linaloshuhudiwa

Nairobi – Serikali ya Sudan Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kwa muda usiojulikana kutokana na wimbi la joto kali ambalo linaweza kusababisha viwango ya joto kuongezeka hadi nyuzi.

Mataifa kadhaa ya dunia yameshuhudia viwango vya juu vya joto ikiwemo Algeria
Mataifa kadhaa ya dunia yameshuhudia viwango vya juu vya joto ikiwemo Algeria AFP - -
Matangazo ya kibiashara

Mamlaka ya afya na elimu kwenye taifa hilo pia imewataka wazazi kuwazuia watoto wao kucheza nje kwa muda mrefu, wakisema joto hilo linaweza kudumu kwa wiki mbili.

Aidha mamlaka hiyo pia imesema kuwa tayari kumeripotiwa vifo vinavyohusiana na joto kupita kiasi.

Kwa mujibu wa mamlaka, shule yoyote itakayopatikana imefunguliwa kuanzia Jumatatu, usajili wake utaondolewa.

Wiki iliyopita, takriban watoto 15 waliripotiwa kufariki kutokana na homa ya uti wa mgongo na magonjwa mengine yanayohusiana na joto, kulingana na wizara ya afya.

Baadhi ya mataifa ya Afrika Mashariki ikiwemo Kenya nayo pia yameripoti ongezeko la viwango vya juu vya joto haswa nyakati za usiku.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.