Viongozi wa Afrika kuipa kipau mbele huduma za afya wakati wa mizozo na majanga
Na Carol Korir, Lusaka
Imechapishwa: Imehaririwa:
Viongozi wa Afrika kwa ushirikiano ya mashirika ya kikanda yanayoangazia afya wamekutana jijini Zambia kwa kongamano la tatu kuhusu afya ya umma ,wito ukitolewa kwa nchi za Sahel kuzingatia utoaji wa huduma za afya licha ya kuathirika na mizozo tofauti.
Kikao hicho kinachoratibiwa na Umoja wa mataifa kwa ushirikiano na shirika la udhibiti magonjwa barani Afrika ,CDC ni muendelezo wa mjadala kuhusu mfumo wa afya barani baada ya janga la Uviko 19.
In the "Defeating Malaria through Equitable Partnerships” Side Event, panel participants emphasized the crucial role of sustainable partnerships in tackling Malaria in Africa. A shared mission unites all partners, making it an opportunity for mutual learning. Advocacy and… pic.twitter.com/2JFkzrzB57
— CPHIA Official (@CPHIA_AfricaCDC) November 27, 2023
Dr Jean Kaseya mkurugenzi wa shiriki la udhibiti wa magonjwa barani Afrika CDC amesisitiza umuhimu wa mataifa ya Afrika ambayo kwa sasa yanashuhudia ongezeko la mizozo ya kisiasa na utovu wa usalama kukumbatia diplomasia katika sekta ya Afya.
Amesema CDC imeanza mkakati kuwasaidia nchi za ukanda wa Sahel ambazo hivi karibuni imekubwa na msururu wa mapinduzi ya kijeshi kukabiliana na hali za dharura katika huduma za afya na mlipuko wa magonjwa hatari.
"Tunahitaji kuwa na uthabiti katika swala la diplomasia katika afya,hata kama unapigana kisiasa,au hata kijeshi,kukiwa na mlipuko wa ugonjwa ,unavunja mipaka bila kujali. Haijalishi ni wakati gani tunastahili kupambana na mlipuko,tunasaidia nchi za Afrika Magharibi kukabiliana na dharura pamoja na nchi zingine." alisema Dkt Kaseya katika ufunguzi wa kongamano la CPHIA katika chumba cha mkutano cha Kennedy Kaunda.
Dr Jean Kaseya kutoka Africa CDC
Rais wa Zambia Hakainde Hichelema akifungua rasmi kikao hicho,amesistiza nguvu ya uongozi katika kufanikishwa sera za afya.
We commend @AfricaCDC & all partners who contribute to health, saving lives & keeping our workforce healthy.
— Hakainde Hichilema (@HHichilema) November 27, 2023
We're grateful for your leadership & encourage you to continue doing good for humanity.#CHPIA2023 pic.twitter.com/X8O0Rh8YoV
Kwa mujibu wa rais Hakainde, bara Afrika kando na kuhitaji nia ya kisiasa inahitaji pia kutambua nafasi ya kuwa mpambanaji.
"Naweza kukudhirishia kuwa katika AU kama viongozi wa Afrika tumejitolea kuhakikishia kuwa tunapata huduma bora za afya,wanapopata wengine." alisisitiza rais Hichelema.
Rais wa Zambia kuhusu CPHIA
Naye mwenyekiti wa waandaji wa kongamano la CPHIA Profesa Magret Gyapong amesisitiza ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi kupambana na magonjwa yaliyochangamoto kwa Afrika.
"Ushirikiano kati ya serikali na sekta ya binafsi pia mashirika ya kiraia, kubadilishana ufahamu na kuweka pamoja rasli mali ,umeboresha ukuaji wa teknolijia katika afya ya umma. Ufanisi kwenye chanjo ya malaria ya RTS ni dhihirsho tosha ya ushirikiano wa wanasayansi wa Afrika pamoja na washirika muhimu kukabilia matatizo ya afya ya Afrika. "alisema profesa Magret.
“CPHIA is a continental platform that brings together all stakeholders to deliberate and share best practices on the 2023 theme of Breaking Barriers: Repositioning Africa in the Global Health Architecture, which will further guide the effective implementation of @AfricaCDC’s… pic.twitter.com/O8TKspEhQC
— Africa CDC (@AfricaCDC) November 27, 2023
Idadi ya mataifa ya Afrika yanayoshuhudia mizozo imezidi kuongezeka kuanzia ukanda wa Sahel,Afrika ya kati na hata Pembe ya Afrika.
“It may seem like a lot for countries to invest in health, but at the end of the day, because the entire country would have access to primary care, the government ends up paying less.” -@agnesbinagwaho on Rwanda’s #UHC program and why #UHC is beneficial for people and governments… pic.twitter.com/I5ZrglktIU
— CPHIA Official (@CPHIA_AfricaCDC) November 27, 2023