Kenya na EU zimetiliana saini makubaliano kuhusu mkataba wa kibiashara baiana yao
NAIROBI – Umoja wa Ulaya na nchi ya Kenya zimetiliana saini makubaliano kuhusu mkataba wa kibiashara baiana yao, hatua inayokuja wakati huu EU ikitafuta uhusiano wa kina wa kiuchumi na Afrika.
Imechapishwa: Imehaririwa:
"Leo ni wakati wa kujivunia sana kwa Kenya, ambapo naamini pia ni wakati wa kujivunia sana kwa Umoja wa Ulaya," Waziri wa Biashara wa Kenya Moses Kuria alisema baada ya kutia saini mkataba wa ushirikiano wa kiuchumi wa EU na Kenya na Kamishna wa Biashara wa EU Valdis Dombrovskis.
The deal assures Kenya of an expanded, stable, lucrative and sustainable market, enhancing trade and investment opportunities. This will create employment for millions of people, expand earnings and spur sustainable growth. pic.twitter.com/rCzGQVbMR2
— William Samoei Ruto, PhD (@WilliamsRuto) June 19, 2023
Mara baada ya kuidhinishwa na kuanza kutumika, mpango huo wa kibiashara unatarajiwa kuipa Kenya kufikia soko la Ulaya ambapo inatuma sehemu kubwa ya mauzo yake nje.
Kenya inatuma bidhaa zake za kilimo kama vile chai na kahawa maarufu nchini humo na asilimia 70 ya maua yake kwa nchi za kigeni.
EU-Kenya Economic Partnership Agreement briefing, State House, Nairobi. https://t.co/PxXJfDQE8b
— State House Kenya (@StateHouseKenya) June 19, 2023
"Hii ni siku muhimu sana kwa uhusiano wa EU na Kenya," Dombrovskis alisema katika hafla iliyohudhuriwa pia na Rais wa Kenya William Ruto na Naibu Rais Rigathi Gachagua.
"Ninatazamia kusonga mbele haraka iwezekanavyo ili kutia saini na kutekelezwa kwa mafanikio kwa mkataba huu ili watu wetu na uchumi kuanza kuhisi manufaa yake."
President @WilliamsRuto: "The EU – Kenya Economic Partnership Agreement also anchors a framework which enables us to direct our strategic focus towards tackling climate change, and further commits the parties to take active measures to promote sustainable trade."
— Hussein Mohamed, MBS. (@HusseinMohamedg) June 19, 2023
~EU-Kenya… pic.twitter.com/mpPl30B9cj
Mkataba huu iliyotia saini Kenya, unafuatia majadiliano ya muda mrefu, ambapo tangu mwaka 2016 nchi wanachama za jumuiya ya Afrika Mashariki zilikataa kutia saini ushirikiano huu kwa kile zilisema utanufaisha zaidi Ulaya kuliko Afrika.