Rais Tshisekedi ahitimisha ziara yake ya kikazi nchini China
NAIROBI – Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Felix Tshisekedi, amemaliza ziara ya siku nne nchini China, alikotia saini mikataba kadhaa ya ushirikiano wa kibiashara na uchumi na mwenyeji wake, XI Jinping.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Cheza - 00:43
Viongozi hao wawili, wameapa kuimarisha zaidi uhusiano kati ya nchi hizo mbili, hasa kwenye maeneo ya kimkamati hasa uwekezaji kwenye sekta ya madini.
Ushikiano zaidi unatarajiwa kushuhudiwa kwenye sekta ya teknolojia, Kilimo, mazingira na elimu.
#RDC 29.05.2023|#HongKong
— Présidence RDC 🇨🇩 (@Presidence_RDC) May 29, 2023
Le président Tshisekedi a échangé ce lundi à #HongKong, dernière étape de sa visite en Chine, avec Li Jiachao, chef du gouvernement de cette région administrative spéciale chinoise, sur le renforcement de la coopération entre la #RDC et #HongKong. pic.twitter.com/tg6qPCtnYs
Kuhusu ushirikiano katika sekta ya madini, macho ni kuhusu namna mataifa hayo mawili sasa yatashirikiana kuhusu mikataba iliyotiwa saini mwaka 2007 ambapo kampuni kutoka China, zinatakiwa kuwekeza lakini makubaliano hayo yajatekelezwa kikamilifu.
Akiwa nchini China, rais Tshisekedi alisisitiza umuhimu wa ushirikiano huu kuyanufaisha kwa usawa mataifa hayo mawili, huku China ikitumai kuwa Kinshasa itahakikisha mazingira ya uwekezaji yanaimarishwa.