Benin: Tume ya uchaguzi inasubiriwa kutangaza matokeo ya uchaguzi wa wabunge
Tume ya uchaguzi nchini Benin, imesema imeendelea kupokea karatasi za kupigia kura kutoka kwenye majimbo mbalimbali ya nchi hiyo, na kwamba zoezi la ujumuishaji matokeo linaendelea na huenda hadi kufikia kesho watakuwa wametangaza matokeo rasmi.
Imechapishwa:
Cheza - 00:35
Ruffin Domingo, ni mkuu wa operesheni za ulinzi wa kura katika tume ya uchaguzi.
“Tunayafungua kwa sasa maboxi haya na kutoa ripoti ya kura zilizopigwa, baadae tunazikusanya katika chumba cha komputa kupata kanzi data zote.”amesema Ruffin Domingo.
Uchaguzi wa mwishoni mwa juma lililopita, unatarajiwa kuwa kipimo kwa rais Patrice Talon, ambapo kwa mara ya kwanza tangu aingie madarakani, upinzani umeshiriki.