Pata taarifa kuu

Washington yatenga dola Milioni 10 kwa atakayesaidia kukamatwa kwa Maalim Ayman

Marekani imeahidi kutoa zawadi ya Dola  milioni 10 , kwa yeyote ,atakayesaidia kukamatwa kwa kiongozi wa kundi la kigaidi la Al Shabab,Maalim Ayman , anayetuhumiwa kuongoza shambulio katika kambi yake eneo la Manda ,Pwani ya Kenya, lilosababishwa vifo vya raia wake watatu pamoja na wanajeshi kadhaa wa Kenya.

Rais wa Marekani Joe Biden wakati wa tangazo la kifo cha kiongozi wa al-Qaeda Ayman al-Zawahiri aliyelengwa katika shambulio la ndege ya Marekani.
Rais wa Marekani Joe Biden wakati wa tangazo la kifo cha kiongozi wa al-Qaeda Ayman al-Zawahiri aliyelengwa katika shambulio la ndege ya Marekani. © Jim Watson/Pool via REUTERS
Matangazo ya kibiashara

Miaka miwili tangu shambulio hilo kwenye kambi ya  Manda , inayokaliwa na wanajeshi wa Marekani êneo la Pwani ya Kenya, Marekani haijasahau tukio hilo na sasa inamsaka kiongozi wa kundi hilo.

Shambulio hilo la  Januari 5 mwaka 2020 ,lilowalenga wanajeshi wa Marekani nchini Kenya lilotokelezwa kutumia roketi.

Maalim Ayman ameendelea kushtumiwa kwa kupanga mashambulio ya kigaidi nchini Kenya na Somalia kwa kipindi cha miaka kadhaa sasa.

Hadi sasa ,Marekani ,imelipa kiasi cha dola  milioni  250 kwa watu 125 waliotoa ushirikiano wa kupatikana ,magaidi wanaotafutwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.