Milipuko Somalia: Al Shabab wamekiri kuhusika
Watu 19 wameuawa kwenye mashambulio mawili ya bomu, katikati ya nchi ya Somalia, mashambulio ambayo magaidi wa Al Shabab wamekiri kutekeleza, na kudai pia kushambulia kambi za jeshi katika miji ya miji ya Mahasa na Dadan Ad.
Imechapishwa:
Kwa mujibu wa kiongozi wa kundi lenye silaha linaloshirikiana na serikali kupambana na magaidi hao katika eneo hilo la Mahasa ,Mohammed Moalim Adan ,waliopoteza maisha ni wanajeshi pamoja na raia, huku wengine 52 wakijeruhiwa.
Kundi hilo limesema mashambulio hayo ya jana yalihusisha ;magari mawili yaliyokuwa na vilipuzi ,yaliyolipuliwa katika mji wa Mahas, iliyokuwa ngome ya Al Shabab kabla ya kutimuliwa mwaka uliopita.
Aidha, Kamanda wa polisi êneo hilo Osman Nur ,amesema , magaidi hao walikuwa wameamua kuwalenga raia wasio na hatia baada ya kuonekana kuzidiwa nguvu kwenye operesheni ya vikosi vya serikali.