Somalia: Tisa waangamia katika milipuko ya mabomu mawili katika Wizara ya Elimu
Nchini Somalia, magari mawili yaliyokuwa na mabomu yamelipuka kwenye afisi ya Wizara ya Elimu ya Somalia Jumamosi hii, Oktoba 29, huko Mogadishu.
Imechapishwa:
"Milipuko miwili ya wakati mmoja" imetokea kwenye barabara kando ya wizara na kusababisha "vifo kadhaa", msemaji wa polisi ya Somalia Sadik Dudishe amesema, na kuongeza: "Tutatoa maelezo zaidi baadaye. Shambulio hili la mabomu mawili liliua takriban watu tisa, kulingana na vyanzo vya usalama.
Shambulio hilo lilitokea mchana na moja ya milipuko hiyo inaripotiwa kukumba afisi za Wizara ya Elimu.
Hadi kufikia sasa, hakuna taarifa zozote zilizotolewa zinazoangazia idadi ya watu waliojeruhiwa wala hakuna aliyedai kuhusika na milipuko hiyo.