Chad - Siasa
Chad: Makundi ya upinzani kushiriki mazungumzo ya amani
Vyama vya upinzani na makundi ya waasi nchini Chad, yamekubali kushiriki mazungumzo ya amani ya nchini Qatar, kinyume na misimamo yao ya awali.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Mapema mwezi huu vyama hivyo vilijiondoa katika mazungumzo hayo, vikituhumu serikali ya kijeshi ya Chad kwa kuwanyanyasa na kuwatisha.
Rais wa mpito, Idris Deby, tayari ametangaza kuanza kwa mazungumzo ya kitaifa ambayo yametajwa kuwa sehemu muhimu kuelekea kuandaliwa kwa uchaguzi.
Kifo cha rais wa muda mrefu wa Chad Idris deby mwaka uliopita, litumbukiza taifa hilo kwa mgorogoro wa kisiasa.