Pata taarifa kuu
BURKINA FASO-SIASA

Wafuasi wa watawala wa kijeshi Burkina Faso waandamana Ouagadougou

Nchini Burkina Faso, kumekuwa na maandamano ya raia kuunga mkono hatua ya jeshi kuchukua madarakani, huku Ufaransa na Umoja wa Mataifa ukilaani hatua hiyo.

Maandamano ya kuunga mkono viongozi wa mapinduzi, huko Ouagadougou, Januari 25, 2022 siku moja baada ya mapinduzi nchini Burkina Faso ambayo yalimpindua Rais Roch Marc Christian Kaboré.
Maandamano ya kuunga mkono viongozi wa mapinduzi, huko Ouagadougou, Januari 25, 2022 siku moja baada ya mapinduzi nchini Burkina Faso ambayo yalimpindua Rais Roch Marc Christian Kaboré. AFP - OLYMPIA DE MAISMONT
Matangazo ya kibiashara

Wanajeshi waliochukua madaraka wanamzuia rais Roch Marc Christian Kabore, wanamshtumu kwa kushindwa kupambana na makundi ya kijihadi nchini humo.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron,amesema analaani hatua hiyo ya mapinduzi na kuongeza kuwa, nchi yake inaunga mkono, msimamo wa Jumuiya ya kiuchumi ya  nchi za Afrika Magharibi ECOWAS, kulaani mapinduzi hayo.

Aidha, amesema amefahamishwa kuwa Kabore hayupo kwenye nafasi ya maisha yake kuhatarishwa, huku akisisitiza kuwa ukanda wa Afrika Magharibi kuendelea kushuhudia mapinduzi kunarudisha nyuma jitihada za kupambana na makundi ya kijihadi na ugaidi.

Naye, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres kupitia msemaji wake Stéphane Dujarric  ametaka kuachiwa kwa rais Kabore.

Luteni Kanali Paul-Henri Sandaogo Damiba aliyejitangaza kiongozi wa nchi hiyo, amesema nchi hiyo sasa iko chini ya vuguvugu jipya la kizalendo lililopewa jina la MPSR.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.