Pata taarifa kuu
MOROCCO-USALAMA

Vita vyapamba moto katika Sahara Magharibi, pande katika mzozo zashtumiana

Kwa mwaka mmoja sasa, wapiganaji wanaotaka kujitenga wa Saharawi kutoka kundi la Polisario wameanza tena operesheni zao za kijeshi dhidi ya jeshi la Morocco, baada ya takriban miongo mitatu ya kusitisha mapigano.

Makao makuu ya shirika la Hilali Nyekundu ya Sahrawi huko Rabouni.
Makao makuu ya shirika la Hilali Nyekundu ya Sahrawi huko Rabouni. © RFI/François Mazet
Matangazo ya kibiashara

Mgogoro usio na ulinganifu ambao wanatumaini utaanzisha tena mazungumzo kuhusiana na eneo hili lenye hadhi linayogombaniwa, katikati ya mvutano wa kidiplomasia kati ya Morocco na Algeria.

Hivi karibuni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa aliashiria kuanza tena mapigano kati ya Morocco na Harakati ya Ukombozi wa Sahara Magharibi ya Polisario katika eneo hilo linalozozaniwa na kutangaza kuwa, hali ya mambo katika eneo hilo mwaka mmoja uliopita imekuwa mbaya kwa kiasi kikubwa.

Morocco inalitambua eneo la Sahara Magharibi kuwa sehemu ya ardhi yake; hata hivyo Harakati ya Polisario ambayo kimataifa inatambuliwa kama mwakilishi wa wananchi wa eneo la Sahara Magharibi, imekuwa ikipigania uhuru wa eneo hilo kwa miaka mingi sasa.

Vita vya kupigania uhuru baina ya harakati ya Polisario na Morocco vilianza mwaka 1975 na  kuendelea hadi mwaka 1991 na kisha pande mbili zilisitisha mapigano kwa upatanishi wa Umoja wa Mataifa.

Katika ripoti yake ya hivi karibuni mbele ya Baraza la Usalama, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa alisema kuwa, Harakati ya Polisario mwezi Novemba mwaka jana baada ya vuta nikuvite na Morocco ilitangaza kuwa haitaheshimu tena mapatano hayo ya usitishaji vita kati yake na Morocco.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.