Pata taarifa kuu
NIGERIA-USALAMA

Nigeria: Zaidi ya wanafunzi 129 waliotekwa nyara waachiliwa

Makumi ya wanafunzi kutoka chuo cha Kiislamu magharibi mwa Nigeria, waliotekwa nyara karibu miezi mitatu iliyopita na sita kati yao waliofariki dunia wakiwa mikononi mwa watekaji nyara, wameachiliwa, mkuu wa shule hiyo ametangaza.

Washukiwa wa visa vya utekaji nyara wakioneshwa mbele ya wakaazi wa Jimbo la Taraba, Nigeria.
Washukiwa wa visa vya utekaji nyara wakioneshwa mbele ya wakaazi wa Jimbo la Taraba, Nigeria. © Daily Trust
Matangazo ya kibiashara

Mnamo Mei 30, karibu watu 200 wenye silaha za kivita walivamia mji wa Tegina, Jimbo la Niger (magharibi mwa Nigeria), na kuwateka nyara wanafunzi 136 kutoka shule ya kibinafsi ya Waislamu Salihu Tanko.

Tangu mwezi Desemba, Nigeria imekumbwa na mfululizo wa visa vya utekaji nyara  katika shule na vyuo vikuu.

Wanafunzi sita wa Tegina walifariki wakiwa mikononi mwa watekaji nyara na wengine kumi na tano waliweza kutoroka mnamo mwezi Juni, kulingana na uongozi wa shule.

"Wanafunzi wote wameachiliwa. Tunawapeleka nyumbani," mkuu wa shule ya Salihu Tanko, Abubakar Alhassan ameliambia shirika la habarila AFP. "Siwezi kutoa idadi kamili kwa sasa. Itabidi tuwaangalie mara tu tutakapofika nyumbani. Lakini hakuna mwanafunzi yeyote aliye mikononi mwa watekaji nyara."

Hakutoa maelezo kuhusiana na kuachiliwa kwa wanafunzi hao au kusema ikiwa walilipa fidia kabla ya kuachiliwa.

Maeneo ya Kaskazini magharibi na katikati mwa Nigeria yanakabiliwa na ongezeko la mashambulio, uporaji na utekaji nyara, vitendo vinavyoendeshwa na magenge ya wahalifu wanaojulikana kijijini kama "majambazi". Lakini mwaka huu, magenge hayo yalianza kulenga wanafunzi kwa kwa kutarajia fidia.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.