Mgombea mkuu wa upinzani Hakainde Hichilema aongoza nchini Zambia
Mgombea mkuu wa upinzani nchini Zambia Hakainde Hichilema amechukua uongozi wa mapema kwenye Uchaguzi wa urais dhidi ya rais Edgar Lungu baada ya Tume ya Uchaguzi kuanza kutangaza matokeo siku ya Jumamosi.
Imechapishwa:
Matokeo ya Tume ya Uchaguzi kutoka maeneo Bunge 15 kati ya 156 yaliyotangazwa Jumamosi asubuhi, yanaonesha kuwa Hichilema anaongoza kwa kura 171,604 dhidi ya rais Lungu ambaye amepata kura 110,178.
As the sun rises on a day of destiny for Zambia, our message to those responsible for counting the votes is simple: “Justice, and only justice, you shall pursue, that you may live and possess the land which the Lord your God is giving you” (Deuteronomy 16:20)
— Hakainde Hichilema (@HHichilema) August 14, 2021
Maeneo bunge 15 aliyopata ushindi Hichilema, ni pamoja na ngome za rais Lungu, ambazo alishinda wakati wa Uchaguzi wa mwaka 2016.
Katika maeneo bunge yenye ushindani mkali kama Chawama jijini Lusaka, chama cha rais Lungu na kile cha Hichilema vyote vimedai kushinda.
Let us continue praying for our nation, that the peace we have known for so many years will hold, and let us remain hopeful that we will emerge stronger and united as a people after this episode.
— Edgar Chagwa Lungu (@EdgarCLungu) August 14, 2021
We are a people of hope and Christ our hope remains faithful. #ZambiaDecides2021 pic.twitter.com/RHKkiILpMH
Matokeo ya mwisho yanatarajiwa kufahamika katika siku chache zijazo huku ushindani mkali ukitarajiwa kati ya rais Lungu na Hichilema.
Katika hatua nyingine, Internet imerejeshwa tena nchini humo na watu wameanza tena kutumia mitandao ya kijamii kama WhatsApp ambayo iliyokuwa imezuiwa siku ya Alhamisi na Ijumaa.