ZAMBIA - MAZISHI
Viongozi mbalimbali watua Lusuka kuhudhuria ibada ya wafu ya Kaunda
Viongozi wa tabaka mbalimbali wamewasili nchini Zambia kuhuduria hafla ya kitaifa ya ibada ya wafu ya aliyekuwa rais wa taifa hilo Kenneth Kaunda.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Mpiganiaji huyo wa uhuru wa Zambia alifariki akiwa na umri wa miaka 97 kutokana na pneumonia.
Jeshi la Zambia limekuwa likiusafirisha mwili wa Kaunda, katika mikowa yote 10 ya taifa hilo ili raia watoe heshima zao za mwisho kwa shujaa huyo wa Africa.
Rais wa Zambia, Edgar Lungu, ametangaza leo na siku ya jumatano siku itayozikwa Kaunda kuwa sikuku ya kitaifa.
Hafla ya mazishi ya Kaunda itahudhuriwa na familia yake na viongozi wachache waliakwa siku ya jumatano juma lijalo.