MOROCCO
Morocco kufungua tena mipaka yake kwa watalii Juni 15
Morocco itafungua tena viwanja vya ndege na bandari zake kwa safari za kimataifa kuuanzia Juni 15, kwa raia wake na kwa raia wa kigeni, Wizara ya Mambo ya nje imetangaza.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Wasafiri wote wataruhusiwa kuingia nchini ikiwa watakuwa wamepewa chanjo dhidi ya COVID-19 au kuonyesha cheti ya vipimo ambacho kinaonyesha kuwa hajaambukizwa virusi vya Corona, wizara imesema katika taarifa.
Morocco ilianza mwezi uliopita kulegeza masharti yaliyowekwa kudhibiti ugonjwa wa COVID-19 , ikiwa ni pamoja na kuruhusu majumba ya sinema na kufunguliwa tena.