Morocco: 28 wafariki katika mafuriko ya kiwanda haramu Tangier
Takriban watu 28 wamekufa baada ya mafuriko katika kiwanda cha nguo kisichotambuliwa na mamlaka nchini Morocco, kwa mujibu wa vyanzo vya serikali, vikinukuliwa na shirika la habari la REUTERS.
Imechapishwa:
Kiwanda hiki kinapatikana chini ya nyumba moja huko Tangier, mamlaka nchini Morocco imebaini, na kuongeza kuwa uchunguzi umeanzishwa ili kujua wahusika wa kiwanda hiki.
Maafisa wa usalama wamesema kuwa watu 18 wameokolewa katika shughuli ya uonkoaji inayoendelea katika eneo la tukio.
Kazi isiyo rasmi nchini Morocco inachukua karibu theluthi moja ya shughuli za kiuchumi zisizo za kilimo na wafanyakazi mara nyingi wanakabiliwa na mazingira magumu ya kufanya kazi.