Pata taarifa kuu
ETHIOPIA

Raia wa Misri, Sudan na Ethiopia wasubiri matokeo ya mazungumzo Kinshasa

Mazungumzo ya siku tatu, kujaribu kutafuta mwafaka wa matumizi ya maji ya Mto Nile kufuatia hatua ya Ethiopia kujenga bwawa kubwa la kuzalisha umeme, yanamalizika leo jijini Kinshasa nchini DRC kati ya wawakilishi kutoka Ethiopia, Misri na Sudan.

Mapema mwezi Julai viongozi wakuu wa Misri, Sudan na Ethiopia walikubaliana kwamba Addis Ababa itachelewesha ujazaji wa bwawa lake lililoko kwenye mto wa Blue Nile hadi mataifa hayo matatu yatakapofikia makubaliano juu ya mgawo wa maji ya mto huo.
Mapema mwezi Julai viongozi wakuu wa Misri, Sudan na Ethiopia walikubaliana kwamba Addis Ababa itachelewesha ujazaji wa bwawa lake lililoko kwenye mto wa Blue Nile hadi mataifa hayo matatu yatakapofikia makubaliano juu ya mgawo wa maji ya mto huo. REUTERS/Tiksa Negeri
Matangazo ya kibiashara

Misri inasema mazungmzo haya yanatoa nafasi ya mwisho kabla ya Ethiopia kuendelea kujaza bwawa lake kwa kutumia maji hayo, ili kufanikisha mradi wake ambao inasema utainufaisha kiuchumi, lakini Misri inasema mradi huo utawakosesha raia wake maji.

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Felix Thisekedi na mwenyekiti wa Umoja wa Afrika ndiye mpatanishi wa mazungumzo hayo.

Chanzo cha mgogoro

Misri na Sudan zinasema ujenzi wa bwawa hilo ambalo limegharimu karibu dola bilioni nne, utapunguza maji yanayofika katika nchi hizo na hivyo kuvuruga maisha ya mamilioni ya watu.

Ethiopia nayo inasisitiza ujenzi wa bwawa hilo ni muhimu kwa ajili ya kueneza umeme katika nchi hiyo ili kuimarisha sekta ya viwanda na pia kuuza bidhaa hiyo katika nchi za nje.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.