Pata taarifa kuu
TOGO-SIASA-USALAMA

Faure Gnassingbe kuwania tena uchaguzi wa urais Togo

Rais wa Togo Faure Gnassingbe amethibitisha kuwania tena urais wakati wa Uchaguzi Mkuu mwezi ujao. Huu utakuwa ni muhula wake wanne kuwania wadhifa huo na kuendeleza rekodi ya fanaili yake kuendelea kuwa madaraka.

Rais wa Togo Faure Gnassingbe katika Ikulu ya rais huko Lom kabla ya kutangaza nia yake ya kuwania urasi kwa muhula wa tatu Aprili 28, 2015.
Rais wa Togo Faure Gnassingbe katika Ikulu ya rais huko Lom kabla ya kutangaza nia yake ya kuwania urasi kwa muhula wa tatu Aprili 28, 2015. AFP PHOTO / ISSOUF SANOGO
Matangazo ya kibiashara

Wabunge nchini Togo mwezi Mei mwaka uliopita, walibadilisha Katiba na kumruhusu Gnassingbe kuwania tena kwa muhula mwingine kati ya mwaka 2020-2025.

Mgogoro wa kisiasa unaoendelea nchini Togo umesababisha mdororo wa kiuchumi, huku baadhi ya maduka yakiendelea kufungwa kutokana na hali mbaya ya kiuchumi. Raia wanaendelea kukabiliwa na hali mbaya ya kimaisha, huku mashirika mbalimbali yakiwataka wanasiasa, hasa serikali kutafutia ufumbuzi mgogoro huo.

Faure Gnassingbe alichaguliwa kwa muhula mwengine mnamo mwaka 2010 na 2015 katika uchaguzi uliozua utata na kususiwa na upinzani, baada ya kumrithi baba yake aliyetawala nchi hiyo kwa kipindi cha miaka 38.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.