Kumi na mbili wauawa katika machafuko mapya Bria Jamhuri ya Afrika ya Kati
Miili ya watu kumi na mbili, ikiwa ni pamoja na miili ya wanawake kumi, imegunduliwa siku wa Alhamisi kuamkia leo Ijumaa asubuhi huko Bria, Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Imechapishwa:
Kwa mujibu wa vyanzo kutoka nchini humo vilivyohojiwa na VOA Afrique, watu hawa waliuawa na kundi la zamani la waasi la Seleka kwa kulipiza kisasi shambulio dhidi ya moja ya misafara yao. Shambulio ambalo linadaiwa kuwa lilitekelezwa na kundi la wanamgambo wa Wakikristo la Anti-balaka kilomita 7 kutoka katika mji wa Bria kwenye barabara inayoelekea Ippy.
Vyanzo hivyo vinasema kwamba watu waliouawa walikua wakimbizi wa ndani kutoka kambi ya PK3, iliyo karibu na kambi ya jeshi la Umoja wa Mataifa nchini humo (Minusca).
Kutokakana na mauaji hayo, watu kadhaa waliokimbia makazi yao wameandamana leo Ijumaa mbele ya kambi ya Minusca wakionyesha uzembe wa kikosi hiki cha Umoja wa Mataifa.
Polisi iliingilia kati na kutawanya waandamanaji hao kwa kutumia gesi za machozi.