Pata taarifa kuu
DRC-UBELGIJI

DRC yasema haitaki tena ushirikiano wa kijeshi na Ubelgiji

Serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo imetangaza kusitisha ushirikiano wake wa kijeshi na Ubelgiji.

Jeshi la DRC  FARDC katika jimbo la Kivu Kaskazini  wakipiga doria mwezi Novemba  2013.
Jeshi la DRC FARDC katika jimbo la Kivu Kaskazini wakipiga doria mwezi Novemba 2013. AFP PHOTO / Junior D. Kannah
Matangazo ya kibiashara

Taarifa zilizotolewa na Radio ya Umoja wa Mataifa ya Okapi, zimesema uamuzi wa serikali ya Kinshasa unakuja baada ya kushuhudia mvutano wa kisiasa wa chini kwa chini kati ya serikali hizo mbili tangu kuteuliwa kwa Waziri Mkuu mpya Bruno Tshibala.

Jarida la kila wiki la Jeune Afrique linalochapishwa nchini Ufaransa siku ya Alhamisi, msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Ubelgiji Laurence Mortier, amesema amepokea taarifa hizo kutoka Kinshasa bila maelezo yoyote.

Aidha, amesema Brussels inaendelea kufanya tathmini ya ushirikiano huo na inataka ufafanuzi zaidi kuhusu hatua hii.

Ubelgiji imekuwa ikisaidia kijeshi nchi ya DRC kwa kuwapa mafunzo wanajeshi wake miongo kadhaa sasa kuwasaidia kupambana na makundi ya waasi.

Ushirikiano huo ulianza kutiwa dosari tangu kuanzishwa kwa Vita vya ukombozi vilivyofanikisha kuwepo utawala mpya chini ya Marehemu rais Laurent Desire Kabila, mwaka 1996 lakini uhusiano huu ukarejeshwa baada ya Joseph Kabila kuingia madarakani.
 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.