Pata taarifa kuu
UFARANSA-TUNISIA

Cazeneuve atembelea Tunisia baada kuondoka Algeria

Waziri Mkuu wa Ufaransa Bernard Cazeneuve anaendelea na ziara yake barani Afrika na siku ya Ijumaa ambapo sasa yupo nchini Tunisia.

Waziri Mkuu wa Ufaransa Bernard Cazeneuve  na mwenzake wa Algeria Abdelmalek Sellal walipokutana siku ya Alhamisi Aprili 6 2017
Waziri Mkuu wa Ufaransa Bernard Cazeneuve na mwenzake wa Algeria Abdelmalek Sellal walipokutana siku ya Alhamisi Aprili 6 2017 REUTERS/Stringer
Matangazo ya kibiashara

Ziara hii inakuja baada ya Cazeneuve siku ya Alhamisi kuzuru katika nchi jirani ya Tunisia na kukutana na Waziri Mkuu mwenzake Abdelmalek Sellal.

Cazeneuve na Abdelmalek wamekubaliana kudumisha uhusiano wa kidiplomasia, kisiasa na kiuchumi hata baada ya serikali ya sasa kuondoka madarakani.

Ufaransa inasalia kuwa taifa la kwanza linalowekeza nchini Algeria.

Kampuni 450 za Ufaransa zipo nchini Algeria na wawakezaji kutoka Paris hutumia Dola za Marekani Bilioni 2 kila mwaka katika uwekezaji wa sekta mbalimbali.

Aidha, Ufaransa pia hivi karibuni ilitangaza kundoa visa kwa wananfunzi wa Algeria wanaopenda kwenda kusoma nchini humo.

Wachambuzi wa siasa wanasema kuwa ziara hii imewapa matumaini raia wa Algeria, ambao wengi wanaishi nchini Ufaransa kuwa uhusiano huu utaendelea kudumishwa.

Wagombea kadhaa wa urais nchini Ufaransa kama Emmanuel Macron na Marine Le Pen walizuru Algeria hivi karibuni na kuahidi kudumisha uhusiano kati ya mataifa haya mawili.

Ufaransa ilikuwa koloni ya Algeria.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.