Sudani Kusini: Riek Machar yuko tayari kukutana na Salva Kiir
Kiongozi wa kundi la waasi wa Sudan Kusini, Riek Machar ameahidi kuwa atashiriki mazungumzo ya amani mjini Addis Ababa, Ethiopia kujaribu kusitisha vita viliyolikumba moja kati ya mataifa mapya zaidi duniani, wakati huu ambapo serikali ya Marekani ikitangaza vikwazo dhidi ya viongozi wa Sudan Kusini.
Imechapishwa:
Akiwa ziarani kwenye nchi hiyo, katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa UN, Ban Ki Moon amezitaka pande mbili zinazokinzana nchini humo kukubali na kukutana ana kwa ana mjini Addis Ababa kuzungumzia mzozo wa taifa hilo ili kunusuru vifo zaidi vya wananchi wasio na hatia.
Akizungumza mara baada ya kukutana na katibu mkuu Ban Ki Moon, rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir amemuahidi kiongozi huyo kuwa yuko tayari kwenda Juba kukutana na mwenzake iwapo naye atafanya hivyo.
Kwa upande wake Katibu Mkuu
Ban Ki-moon is in #SouthSudan today. Photos & more info from @unmisspio are here: https://t.co/sNtUwJYm7i pic.twitter.com/TCu4t6Ftmd
— United Nations (@UN) May 6, 2014
Ban, anasema kuwa amefanya kila linalowezekana kuwashawishi viongozi hawa na kwamba alizungumza kwa njia ya simu na Riek Machar na kumpa hakikisho la kuhudhuria mazungumzo ya amani mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Hatua hii inafikiwa huku nchi ya Marekani hapo jana ikitangaza vikwazo dhidi ya Marial Chanuong kamanda wa kikosi maalumu cha rais pamoja na Peter Gadet kiongozi wa kundi la wapiganaji wanaopinga uasi kwenye nchi hiyo.
Mapigano kati ya jeshi linalomuunga mkono raia Salva Kiir na waasi wanao muunga mkono, Riek Machar, aliekua makamu wa Salva Kiir, yamesababisha vifo vya maelfu ya watu huku watu zaidi ya 500.000 wakihama makaazi yao.