Pata taarifa kuu

Urusi: Alexei Navalny mkosoaji wa rais Putin amefariki akiwa jela

Nairobi – Kiongozi mkuu wa upinzani nchini Urusi, Alexei Navalny, amefariki dunia akiwa gerezani, kwa mujibu wa ripoti za maafisa wa Magereza alikokuwa amefungwa.

Russian opposition leader Alexei Navalny, who was detained at a recent protest called under the slogan "Putin is not our tsar", attends a court hearing in Moscow, Russia May 15, 2018
Alexei Navalny, mwanasiasa wa upinzani nchini Urusi amefariki REUTERS - Tatyana Makeyeva
Matangazo ya kibiashara

Ripoti za kutoka kwenye huduma ya magereza zimesema, Navalny alijisikia vibaya ghafla  baada ya matembezi siku ya Ijumaa na kupoteza fahamu, na jitihada za kumzindua hazikufua dafu.

Aidha, maafisa nchini Urusi wanasema wanachunguza kufahamu nini kilichomuua mwanasiasa huyo maarufu wa upinzani.

Navalny alifungwa jela miaka 19, tangu mwaka 2021, baada ya kupatikana na makosa ya rushwa na wizi wa Dola Milioni 4.7 zilizokuwa zitumike kwenye mashirika yake ya kisiasa, aliyopinga.

Amekuwa mkosoaji mkubwa wa sera za rais Putin
Amekuwa mkosoaji mkubwa wa sera za rais Putin © Madiazona/Alexandra Astachova

Mwaka uliopita, alihamishiwa kwenye  gereza la Arctic, linaloaminiwa kuwa na ulinzi mkali kwenye jimbo la Siberia.

Hata hivyo, mashtaka dhidi ya mwanasiasa huyo, yamekuwa yakiaminiwa kuchochewa  kisiasa kwa sababu ya ukosoaji wake kwa rais Vladimir Putin.

Baadhi ya viongozi wa nchi za Magharibi wamemhusisha rais Putin na kifo cha mwanasiasa huyo
Baadhi ya viongozi wa nchi za Magharibi wamemhusisha rais Putin na kifo cha mwanasiasa huyo AFP - ALEXANDER KAZAKOV

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz amesma Navalny, amelipitia ujasiri wake kupoteza maisha yake, huku Katibu Mkuu wa Jeshi la NATO Jens Stoltenberg akisema kuna maswali mengi kuhusu kifo cha mwanasiasa huyo.

Navalny, aliwahi kuponea kifo bada ya kupewa sumu lakini akatibiwa nchini Ujeurumani na baadaye kuamua kurejea Urusi alipokamatwa jijini Moscow.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.