Ufaransa: Waziri Mkuu Élisabeth Borne awasilisha barua ya kujiuzulu kwa serikali yake
Waziri Mkuu wa Ufaransa Elisabeth Borne amewasilisha barua ya kujiuzulu kwa serikali yake siku ya Jumatatu Januari 8, 2023, na kukubaliwa na Rais Emmanuel Macron ambaye alimshukuru kwa kazi yake "ya mfano" kwa "hudumia taifa". Katika muda wa miezi 20 akiwa mkuu wa serikali, Élisabeth Borne alifanya mageuzi ya pensheni ambayo hayakupendwa sana na sheria yenye utata ya uhamiaji.
Imechapishwa:
Siku ya Jumatatu Waziri Mkuu Élisabeth Borne amebaini kuwa "ilikuwa muhimu zaidi kuliko hapo awali kuendelea na mageuzi" katika barua yake ya kujiuzulu aliyomkabidhi Emmanuel Macron. "Wakati ninalazimika niwasilishe barua ya kujiuzulu kwa serikali yangu, nilitaka kukuambia jinsi nilivyokuwa na shauku juu ya misheni hii, nikiongozwa na wasiwasi wa mara kwa mara, ambao tunashiriki, kufikia matokeo ya haraka na yanayoonekana kwa wananchi wenzetu," ameandika Élisabeth Borne, akibainisha "nia" ya Mkuu wa Nchi "kumteua Waziri Mkuu mpya".
Katika ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa X (zamani ukiitwa Twitter), Emmanuel Macron amemshukuru Waziri Mkuu kwa "moyo mkunjufu" kwa kazi yake ya "mfano" "kwa kuhudumia taifa"
Élisabeth Borne na timu yake watashughulikia masuala ya kila siku hadi kuteuliwa kwa serikali mpya.
Madame la Première ministre, chère @Elisabeth_Borne, votre travail au service de notre Nation a été chaque jour exemplaire. Vous avez mis en œuvre notre projet avec le courage, l’engagement et la détermination des femmes d’État. De tout cœur, merci. pic.twitter.com/G26ifKfKzj
— Emmanuel Macron (@EmmanuelMacron) January 8, 2024
Yule ambaye amekuwa katika serikali zote tangu 2017 anaamini katika barua yake ya kujiuzulu kwamba "ni muhimu zaidi kuliko hapo awali kuendelea na mageuzi ili kutoa fursa na mitazamo kwa kila mtu ndani ya Jamhuri na kujenga Ufaransa yenye nguvu na ya haki katika Ulaya iliyo na uhuru zaidi. .”
Bi. Borne alilazimika kukabiliana na takriban hoja thelathini za kushutumu na akatumia kifungu cha 49.3 cha Katiba mara 23. Katika barua yake, hata hivyo, amefurahi kupitisha "katika mazngira ambayo hayajawahi kushuhudiwa katika Bunge, nakala ya kifedha, pamoja na mageuzi ya pensheni, sheria inayohusiana na uhamiaji, na zaidi ya sheria hamsini zinazojibu changamoto za nchi yetu na mashaka ya Wafaransa."
"Mbali na nakala ya kifedha, tuliweza kujenga miradi mingi kwa nia ya kushinda uchaguzi wako mwaka wa 2017," anasisitiza Bi. Borne, ambaye alilazimika kushughulika kwa muda wa miezi ishirini pamoja na waliowengi katika Bunge kutokana na uchaguzi wa wabunge wa mwezi Juni 2022.
Pia alisema "anajivunia kwamba Ufaransa sasa ina mipango kamili na thabiti ya ikolojia", iliyowasilishwa mwezi Septemba mwaka uliyopita.
Ugumu wa kuanzisha uhusiano na Wafaransa
Mwenye busara, wakati mwingine mkali kupita kiasi, mara nyingi akiwa na sigara ya kielektroniki mdomoni, gavana huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 62 ndiye mwanamke wa pili kuchukua nafasi hii. Atakuwa amevuka kwa kiasi kikubwa muhula (miezi 10 na siku 18) ya mtangulizi wake Édith Cresson, aliyeteuliwa zaidi ya miaka thelathini iliyopita.
Lakini mwanamke huyu anayejulikana kama maarufu hata kukosa huruma, alijitahidi kuanzisha uhusiano na Wafaransa na alijikuta katika mzozo na rais.