Pata taarifa kuu

Mafuriko nchini Italia yaua watu 14, 'bustani' ya nchi hiyo ikiwa imeharibiwa

Idadi ya waliofariki kutokana na mafuriko imeongezeka hadi 14 huko Emilia-Romagna, eneo tajiri linalochukuliwa kuwa "bustani ya matunda ya Italia". Uharibifu wa nyenzo na kilimo pia ni wa kiwango cha nadra, ishara, kulingana na mamlaka, ya mabadiliko ya hali ya hewa yanayoendelea.

Kwa sababu ya hali mbaya ya hewa, miji kadhaa ya nyanda za chini imefurika, zaidi ya watu 13,000 wamelazimika kuhamishwa na
Nyumba 50,000 hazina umeme.
Kwa sababu ya hali mbaya ya hewa, miji kadhaa ya nyanda za chini imefurika, zaidi ya watu 13,000 wamelazimika kuhamishwa na Nyumba 50,000 hazina umeme. AP - Luca Bruno
Matangazo ya kibiashara

Idadi ya watu waliofariki kutokana na mafuriko yanayoikumba Emilia-Romagna imeongezeka. Takriban watu 14 wamefariki katika eneo hili tajiri la kilimo na kitalii kaskazini mwa Italia, viongozi wa eneo hilo wamesema Ijumaa Mei 19.

Waokoaji bado walikuwa wakifanya kazi ya kuwahamisha watu waliokwama katika nyumba zao zilizozingirwa na mafuriko na mvua ilianza kunyesha tena baada ya zaidi ya saa 24 za utulivu.

Huko Ravenna, viongozi wameagiza "kuondoka haraka" katika maeneo kadhaa Ijumaa asubuhi na kutoa wito kwa raia "kuhama tu ikiwa ni lazima".

(Pamoja na AFP)

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.