NEW ZEALAND- SIASA
New Zealand: Waziri mkuu Jacinda Ardern kujiuzulu mwezi ujao
Waziri Mkuu wa New Zealand, Jacinda Ardern, ametangaza kuwa atajiuzulu mwezi ujao, kufuatia kile anachosema hana nguvu za kuendelea kuwa kiongozi wa nchi hiyo.
Imechapishwa:
Cheza - 00:30
Matangazo ya kibiashara
“Natangaza sitawania tena nafasi ya uwaziri mkuu na nitaondoka katika ofisi kama waziri mkuu mwezi Februari.”
Tangazo lake linakuja baada ya chama chake cha Labour kuonekana kuanza kupoteza umaarufu.
Ardern, ambaye amekuwa madarakani kwa karibu miaka sita, atakumbukwa kwa namna alivyoongoza nchi yake kukabiliana na maambukizi vya Uviko 19, nchi yake ikiandikisha idadi ndogo ya maambukizi.