Pata taarifa kuu

Urusi: Vladimir Putin afutilia mbali mkutano wake wa kitamaduni na waandishi wa habari

Kremlin ilitangaza Jumatatu, Desemba 12, kwamba Rais wa Urusi Vladimir Putin hatafanya mkutano wake wa jadi wa mwisho wa mwaka na waandishi wa habari. Muktadha wa vikwazo vya kijeshi vilivyokusanywa na Urusi nchini Ukraine na vikwazo vya nchi za Magharibi vilivyowekwa dhidi ya Moscow bila shaka havihusiani na uamuzi huu.

Rais wa Urusi hatafanya mkutano wake wa jadi wa mwisho wa mwaka na waandihi wa habari.
Rais wa Urusi hatafanya mkutano wake wa jadi wa mwisho wa mwaka na waandihi wa habari. Russian Presidential Press Service
Matangazo ya kibiashara

"Mwanzoni mwa mwaka mpya, hakutakuwa na" mkutano wa waandishi wa habari na rais, msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov amesema katika mkutano wa simu, akibainisha kuwa Bw Putin alizungumza na waandishi wa habari katika matukio mengine, hasa wakati wa safari zake nje ya nchi. Mkutano huu mkubwa wa ana kwa ana wa kiongozi huyo wa Urusi na waandishi wa habari ulikuwa umeandaliwa kila mwaka tangu 2001, isipokuwa kipindi cha kati ya mwaka wa 2008 na 2012, aliposhikilia wadhifa wa Waziri Mkuu.

Mamia ya waandishi wa habari

Kuleta pamoja mamia ya waandishi wa habari wa Urusi na wa kigeni, mkutano huu wa waandishi wa habari wa kila mwaka kwa kawaida huchukua saa kadhaa, huku Vladimir Putin akijibu maswali ya moja kwa moja juu ya kila aina ya mada, kutoka kwa diplomasia hadi masuala ya kila siku ya Urusi. Majibu ya rais kwa vyombo vya habari mara nyingi yalikuwa sawa na maagizo yaliyotolewa kwa serikali au mamlaka ya kikanda.

Mvua ya vikwazo

Uamuzi wa kutofanya mkutano na waandishi wa habari wa mwisho wa mwaka unakuja wakati Urusi, ambayo ilianzisha mashambulio ya kijeshi dhidi ya Ukraine mnamo mwezi Februari, imekumbwa na vikwazo kadhaa vya kijeshi katika miezi ya hivi karibuni na kutangza uhamasishaji wa watu kungana na jeshi mnamo mwezi Septemba 2022. Urusi ambayo inakabiliwa na vikwazo tangu kuanza kwa mashambulizi haya, sasa inakumbwa na vikwazo vya kuwasilisha mafuta yake kwa Umoja wa Ulaya.

(Pamoja na AFP)

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.