Pata taarifa kuu
ITALIA-COVID 19

Italia yafungwa kipindi chote cha sikukuu ya Pasaka

Nchi ya Italia imefungwa kwa siku tatu, katika kipindi hiki cha pasaka ili kupambana na ongezeko la maambukizi ya Covid 19.

Raia wa Italia wakiwa makwao katika kipindi hiki cha Covid 19
Raia wa Italia wakiwa makwao katika kipindi hiki cha Covid 19 AP - Andrew Medichini
Matangazo ya kibiashara

Hatua hii imekuja baada ya nchi hiyo kuanza kuripoti visa vya maambukizi 20,000  kila siku, katika siku za hivi karibuni.

Maeneo yote ya nchi hiyo sasa yapo katika hali ya hatari kuafutia ongezeko hilo.

Watu wamezuiwa kutembea, lakini wameruhusiwa kushiriki chakula cha pamoja nyumbani siku ya Pasaka.

Makanisa hayajafungwa lakini waumini, wameshauriwa kuhudhuria ibada katika maeneo wanayoishi.

Kwa mwaka wa pili, kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis atalazimika kutoa mahubiri yake siku ya Jumapili kwenye uwanja mtupuu wa Mtakatifu Peter, mjini Vatican kufuatia janga la Covid 19.

Tangu kuzuka kwa maambukizi ya corona, watu zaidi ya Laki Moja na Elfu 10 wamepoteza maisha na wengine zaidi ya Milioni 3.6 wameambukizwa.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.